KAMATI YA MIPANGO NA UCHUMI

PAROKIA YA BIKIRA MARIA WA MLIMA KARMEL - BUNJU
KWAYA YA BIKIRA MARIA WA MLIMA KARMEL
JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM
P. O. Box 167, Dar es Salaam
MOBILE: +255784 799 455

RISALA YA KWAYA KATIKA   MAADHIMISHO YA SOMO WA KWAYA TAREHE 26.07.2015
Utangulizi:

Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Baba Paroko, Mapadre, Ndugu viongozi wa Parokia, Kigango, na viongozi wa vyama vya kitume. Ndugu Wapendwa Walezi, Marafiki wa Kwaya, Ndugu wa Karibu wa wanakwaya na wanakwaya wote. 

 TUMSIFU YESU KRISTO…………………….

Ni jambo Jema na la kumshukuru Mungu aliye asili ya mema yote ambaye ametuwezesha kukaa hapa leo na kuweza kutujaalia  nguvu na ushirikiano wa pamoja wa hali na mali katika Kwaya yetu.

Leo ni siku ambayo tunaadhimisha Somo na Msimamizi wa Kwaya yetu Bikira Maria wa Mlima Karmeli ambapo huwa inaadhimishwa Tarehe 16.07 kwa kila mwaka, hivyo kwa furaha kubwa tunapenda kuwakaribisha ninyi nyote kushiriki nasi katika furaha hiyo kubwa . Tunasema KARIBUNI SANA.

Risala hii imegawanyika katika sehemu zifuatazo:-

1.     HISTORIA FUPI YA KWAYA

Kwaya ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli ilianzishwa mnamo mwaka 1998 ikiwa chini ya Somo na Msimamizi wa Kwaya Mt. Fransisko wa Asizi ikiwa na wanakwaya waanzilishi 15. Na baadaye kubadilisha jina na kuwa chini ya Somo na Msimamizi Mama Bikira Maria wa Mlima Karmeli mnamo mwaka 2012. Kwa sasa Kwaya ina wanakwaya 55 na inaongozwa na kamati tendaji inayoundwa na viongozi wafuatao:-
  1. Luambano Patrick – Mwenyekiti
  2. Isack Ntalyoka – M/ Mwenyekiti
  3. Sibilina Kimaro – Katibu
  4. Isack Ntalyoka – M/ Katibu
  5. Clara Samwel – Mhazini.
Kwaya pia ina Walezi walei wanane(8) Marafiki wa Kwaya Familia 30.



2. MPANGO KAZI WA MWAKA 2015/2016

Kwa Mwaka 2015, Kamati tendaji ya Kwaya na wanakwaya wote wameridhia kuwa na MPANGO KAZI unaotekelezeka  wa mwaka mzima na kujitahidi kuondoa mgangano/muingiliano wa matukio na vyama vingine vya kitume ili kuweza kuleta ufanisi zaidi kwa kugawanya matukio katika sehemu kuu nne kama ifuatavyo:-
*      Imani na Liturujia
*      Uimbaji
*      Uchumi
*      Mahusiano


1.      IMANI NA LITURUJIA.

v  Katika kuhakikisha wanakwaya wanapata tafakari juu ya imani na wanahudumu kulingana na liturujia kamati tendaji inapendekeza kuwa na  Mafungo pamoja na semina kwa wanakwaya wote yatakayo fanyika mara tatu(3) kwa mwaka yaani:-
i.                    Kipindi cha Kwaresma
ii.                  Kipindi cha Maandalizi kukaribia kuadhimisha Somo wa Kwaya Bikira Maria wa Mlima Karmeli Tarehe 16.07.2015
iii.                Katika Kipindi cha Majilio.
v  Kwa Imani yetu Kamati Tendaji tunaamini kuwa ni kwa uweza wa Mungu tu ndio tunaweza kuhudumu vizuri kadiri ya Liturujia katika Ibada ya Misa Takatifu na Matukio mbalimbali, Hivyo Kwaya  imependekeza kuwa SALA MAALUMU ili kwa pamoja kuweza kujinyenyekeza katika Uweza wa Mungu kila kabla ya kutoa Huduma popote pale.
v  Kuhamasisha na kupanga mikakati ya kuhakikisha kuwa Wankwaya wote wanashiriki Ibada ya Misa Takatifu na Baba Kardinali siku JUMATATU YA PASAKA ambayo ni siku ya Wanashikwaka –Jimbo kukutana na Baba Kardinali, Pia kujifunzaa mambo mbalimbali yahusuyo utume wa Kwaya. 06.04.2015 katika Parokia ya Kipawa.

2.      UIMBAJI/MUZIKI.
Kamati tendaji ya Kwaya katika kuhakikisha tunaboresha uimbaji inapendekeza kufanya mambo yafuatayo:-
A.    Kwa ushirikiano wa Wanakwaya wote na hasa Kamati ya Ufundi kukusanya na kuandaa VITABU NA BAHASHA za nakala za nyimbo mbalimbali kulingana na vipindi mbalimbali vya Liturujia kwa Mwaka mzima.  Yaani kuweka nyimbo katika makundi yafuatayo:-
i.                    Nyimbo za Mwanzo
ii.                  Nyimbo za Misa
iii.                Nyimbo za Zaburi(Katikati)
iv.                Shangilio na Maombi
v.                  Komunio na Ekaristi Takatifu
vi.                Sadaka/Matoleo na Vipaji
vii.              Nyimbo za Kristu Mfalme, Majilio na Krismasi
viii.            Nyimbo za Kwaresma Matawi na Pasaka
ix.                Skukrani na Bikira Maria
x.                  Pentekoste na Kipaimara
xi.                Ubatizo na Ndoa
xii.              Nyimbo za Watakatifu, Tafakari na Misa.
B.     Kuandaa Semina na Mafunzo yanayohusu Elimu ya Muziki, Uongozi na Upimishaji kwa Kamati ya Ufundi na Wanakwaya wengine watakaohitaij ili kuweza kuboresha zaidi Mazoezi yetu, Uimbaji wetu na utoaji wa huduma kwa ujumla.
C.     Kuendelea na zoezi la Kuhamasisha waamini mbalimbali katika Parokia yetu kujiunga na Kwaya ili kuweza kufikia Idadi ya Wanakwaya 70, Kamati pia inapendekeza zoezi la Pili la Kuanzia Saa Moja Kamili(1:00) lifufuliwe ili kutoa fursa na Wigo Mpana wa Kila mwanakwaya kushiriki mazoezi Kikamilifu na kuongeza uwezekano wa kupata Idadi kubwa ya Wanakwaya wapya.
D.    Kuwa na Ziara za Uinjilishaji za Mara kwa Mara ili kuimarisha Kwaya Kiumbaji na kupata fursa ya kujifunza mengi kutoka kwa wenzetu ndani na nje ya Parokia yetu na hata nje ya Jimbo Letu.
E.     Kuandaa na Kuanzisha Darasa La Muziki kwa wanakwaya ili kupata Elimu ya kutuwezesha Kusoma Musiki katika Nota na Kupiga Kinanda.

3.      UCHUMI.
Ili kuweza kutengeneza, Kuinua na Kuimarisha hali ya kiuchumi ya Kwaya na Wanakwaya kwa Ujumla Kamati inapendekeza yafuatayo yafanyike:-

A.    KUWEKEZA FEDHA SACCOS
Ndugu wanakwaya, kamati inapendekeza kuchukua sehemu ya kiasi cha Fedha ya Kwaya iliyopo Benki na Kuiwekeza Katika Mojawapo ya Saccos zilizopo katika Mazingira yetu ili kuweza kuiongezea Uwezo wa Kuichumi wa Kwaya, maana Kwa kuweka fedha Saccos inakupa fursa za Kukopa Mara Tatu(3) ya Amana yako.

B.     KUJIUNGA KATIKA VIKOBA.
Kamati inapendekeza pia sehemu ya Mapato ya Fedha inayoendelea kuyapokea tuwekeze katika Mojawapo ya Vikundi vya Vikoba Vya WAWATA hapa Kanisani. Ili litatupa fursa ya Kupata Faida mwisho wa Mwaka lakini pia Fursa ya Kukopa kadiri ya Mahitaji yetu kwa kiwango cha Hisa za Kikundi. Lakini katika hili kamati ilishauri Wanakwaya mmoja mmoja au katika vikundi nao kujiunga katika Vikoba kwa Imani kuwa ni fursa ya kipekee na yaweza kuchangia kujikwamua kuichumi na kuboresha mahusiano.

C.     ZIARA ZA KUUZA ALBAMU ZETU.
Rejea Maelezo ya Sehemu ya 3.D hapo juu, Kamati inapendekeza pia tuwe na Ziara kwa Lengo la kuendelea Kuuza Albamu Zetu katika mtiririko ulioelezwa hapo juu.

D.    KUTENGENEZA/KUNUNUA VITU NA KUVIUZA.
Kwaya imeazimia kuwa Wabunifu kwa Kutengeneza/ kununua vitu vyenye kuhitajika kwa wanakwaya , familia ya kwaya ya BMMK na Waamini wenye mapenzi mema ili kuinua na kiimarisha Uchumi. Vifuatavyo ni Baadhi ya vitu vilivyopendekezwa:-
*      Kutengeneza /Kununua Sare ambazo baadhi ya wanakwaya  hawana na kwa ziada ili kununuliwa na wanakwaya Wapya.
*      Kubuni Vazi la Familia ya Kwaya ambalo litavaliwa kwenye matukio makubwa ya kwaya yetu Mf. Sherehe ya Maadhimisho ya Somo wa Kwaya n.k. Na litavaliwa na Wanakwaya Wote, Walezi wa Kwaya, Marafiki wa Kwaya na Familia ya Mwanakwaya yaani Mke/Mme/Mtoto/Mlezi…

E.     KUANDAA ALBAMU YA AUDIO NA VIDEO
Katika mwaka kipindi hichi cha mwaka Kwaya imepanga kupanua wigo wa Uinjilishaji kwa Kuandaa Albamu ya Audio na Video. Ambapo Jedwari hapo chini laonesha mchanganuo wa gharama zake:-







A: KUREKODI ALBAMU YA AUDIO
B: KUREKODI ALBAMU YA VIDEO
S/No.
MAHITAJI
 GRARAMA(Tshs.)
S/No.
MAHITAJI
 GRARAMA(Tshs.)
1
NYIMBO 10@20,000
                  200,000
1
MWALIMU WA STAILI/STEP
                       500,000
2
STUDIO
                  600,000
2
STUDIO
                    3,000,000
3
KUKODI KINANDA
                  150,000
3
MAVAZI(SARE) JOZI 4 X 55@40,000
                    8,800,000
4
MPIGA KINANDA
                  150,000
4
SEHEMU ZA KUREKODIA
                       500,000
5
NAULI KWENDA STUDIO
                  100,000
5
USAFIRI KWA SIKU 3@200,000/=
                       600,000
6
CHAKULA STUDIO 55@2000
                  110,000
6
CHAKULA KWA SIKU 4 *55@4000
                       880,000
7
DHARULA
                     90,000
7
JENERETA NA MUSIKI
                       300,000



8
DHARULA
                       420,000






JUMLA
    1,400,000
JUMLA
      15,000,000


4.      MAHUSIANO.
Kamati inapendekeza yafuatayo yafanyike ili kuamsha na kuboresha mahusiano kati ya :-
§  Wanakwaya Wenyewe
§  Wanakwaya, Walezi, Marafiki na Familia za Kwaya.
§  Wanakwaya na Waamini wote/ Jamii yote ndani na nje ya Parokia yetu.

A.    KUAMSHA NA KUBORESHA KIKUNDI CHA MARAFIKI WA KWAYA.
Kamati inapendekeza kuamsha kundi la Marafiki wa Kwaya kwa wale waliolala na pia kuboresha kwa kuongeza Idadi yao na kuwashirikisha Matukio na Mambo mbalimbali ya Kwaya kwa njia ya UTANDAWAZI. Hivyo kwaya imeridhia kufanya yafuatayo:-
·         Kuwa na Nembo ya Kwaya yenye kujumuisha Anuani ya Kwaya, Barua pepe na Namba za simu
·         Kuwa na E- mail ya Kwaya.
·         Kuwa na Blog ya Kwaya ambayo itakuwa na vitu vifuatavyo:-
i.                    Picha na video za Matukio Mbalimbali ya Kwaya
ii.                  Picha za Wanakwaya, Walezi, Marafiki na Majina yao
iii.                Kauli mbiu ya Kila Mwanakwaya
iv.                Katiba ya Kwaya
v.                  Historia ya Kwaya
vi.                Albamu za Kwaya na Miradi yake
vii.              Ratiba za Matukio mbalimbali ya Kwaya Mf. Ibada n.k
viii.            Na vinginevyo vingi.


3. MAFANIKIO YA KWAYA KWA KIPINDI CHA 2015/2016.

A.    UBORESHAJI WA UIMBAJI.
Katika jambo hilo Kwaya imefanikiwa kuanzisha Darasa la Muziki na baada ya kusuasua na Mkufunzi wa kwanza kamati tendaji kupitia kwa Mwenyekiti ilifanya maamuzi ya kubadilisha mwalimu ambapo kwa sasa Mwl. Anthony Kasomangila ndiye anaendelea kufanya mafunzo katika Darasa hilo.

 Katika kufanikisha mpango kazi huo Kwaya inamwezesha Mwalimu wa Darasa hilo la Muziki jumla kiasi cha Tshs. 100,000/= kwa mwezi, kwa kipindi cha miezi miwili katika mchanganuo ufuatao:-
1.      Kwa kuwa tayari wanafunzi 16 tayari wameshajiandikisha na kuanza kusoma, hivyo kila mmoja anapaswa kuchanga Tshs. 5000/= ili kupata 16@5,000/    = 80,000/=.
2.      Na katika Mfuko wa Kwaya tutatoa Tshs. 20,000/= kwa mwezi kwa kipindi cha miezi miwili. Ambao ndio muda wa kozi hiyo.


B.     MAFUNGO YA KWAYA.
Tulifanikiwa kufanya mafungo ya Kwaya ambapo yaliongozwa na Padre mnamo Tarehe 16.05.2015 na yalifanyika nyumbani kwa Rafiki wa Kwaya Mama Theresia Amon.



  1. KUSHIRIKI ADHIMISHO LA MISA YA WANAKWAYA JIMBO JUMATATU YA PASAKA.
Kwaya tulifanikiwa kushiriki na wanakwaya wenzetu wa Jimbo kuu la Dar Es Salaam siku ya jumatatu ya Pasaka Tarehe 06.04.2015. Ambapo maadhimisho hayo yaliongozwa na Mhadhama Kardinali Polycarp Pengo  na yalifanyika katika Parokia ya Kipawa. Hivyo tunapenda kutumia fursa kutoa shukrani zetu za dhati kwa Baba Paroko kwa kutuwezesha kushiriki katika adhimisho hilo.

D.    SALA MAALUMU YA KIKUNDI
Jukumu hilo la kuandaa sala maalumu, Kwaya imeandaa mapendekezo ya sala na inatakiwa ifanyiwe uhakiki na maboresho kwa kuikabidhi katika kamati ya Liturujia na kamati kuipeleka kwa Mapadre ili kuihakiki.

  1. UIMBAJI NA MUZIKI
Kwaya imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutekeleza mikakati yote iliyojiwekea kuhusu Uimbaji na Muziki kwa kufanya yafuatayo:-
  1. Kundaa nyimbo za Vipindi mbalimbali Vya Liturujia ya Kanisa
  2. Kufanya Ziara za Uinjilishaji ndani ya Jimbo letu.
  3. Kuanzisha Darasa la kufundisha wankwaya Upimishaji.
  4. Kuendelea Kuhamasisha Watu mbalimbali kujiunga katika Utume huu wa Uimbaji ambapo kwa sasa tupo wanakwaya 55. Hivyo Bado tunahitajika kuhakikisha kuwa wanakwaya tulionao wanakuwa hai siku zote na Kuongeza wapya ili kufikia malengo yetu ya wanakwaya 70 kwa mwaka huu.

  1. KUJIUNGA KATIKA VIKOBA.
Kwaya tumefanikiwa kujiunga katika mojawapo ya VIKOBA vinavyoendeshwa na WAWATA hapa Parokiani kwetu.

  1. KUTENGENEZA/KUNUNUA VITU NA KIVIUZA

Kwaya imefanikiwa Kubuni Vazi la Familia ya Kwaya ambalo litavaliwa kwenye matukio makubwa ya kwaya yetu Mf. Sherehe ya Maadhimisho ya Somo wa Kwaya n.k. Na litavaliwa na Wanakwaya Wote, Walezi wa Kwaya, Marafiki wa Kwaya na Ndugu mmoja wa karibu wa Mwanakwaya yaani Mke/Mme/Mtoto/Mlezi…. Ambapo  vazi hilo tunapenda kulizindua rasmi siku ya leo. Thamani vya Vazi itajumuisha gharama halisi ya Vazi na gharama nyingine kuchangia utekelezaji na Maendeleo ya Kwaya hasa Mkakati wa Kurekodi Audio na Video ambapo gharama zake ni Tshs.16,400,000/=
  1. MAHUSIANO
Katika kudumisha na kuboresha Mahusiano kati ya Makundi yanayounda Familia ya Kwaya, Tumefanikiwa kuandaa
E-mail na Blog ya Kwaya ambayo itatoa nafasi ya kushirikishana mambo mbalimbali kwa wakati, na pia kupokea mapendekezo/maoni kutoka kwa watu mbalimbali.

  1. CHANGAMOTO ZA KWAYA.

  1. HALI NGUMU YA KIUCHUMI KWA WANAKWAYA
Hali ya kiuchumi kwa wanakwaya bado imekuwa tatizo kiasi kwamba inapelekea hata uhudhuriaji wa mazoezi kuwa sio mzuri kutokana na pilika za utafutaji riziki na hasa usio katika mfumo rasmi, kwani mara nyingi idadi yetu huwa kubwa sana lakini wanakwaya hai ni wachache ambapo kwa sasa ni wanakwaya 40.



  1. KUTOKUWA NA KINANDA CHA KUJIFUNZIA
Vyombo vya Muziki hasa kinanda cha kujifunzia pia ni tatizo katika Kwaya yetu, hivyo kunyima fursa kwa wanakwaya hasa walio katika Darasa la Muziki kujifunza.

  1. IDADI NDOGO YA WANAKWAYA WATU WAZIMA

Kuwa na Idadi ndogo ya wanakwaya Watu Wazima bado Kwaya inaona kama ni tatizo kwani tunaamini kuwa iwepo wao utaweza kuimarisha na kuboresha Kwaya yetu, kwani asilimia kubwa yao watakuwa na Makazi ya kudumu katika Parokia yetu.

  1. MAPENDEKEZO

  1. FURSA YA KUWA NA MARAFIKI WA KWAYA
Kutokana na hii fursa ya uwepo wa Marafiki wa Kwaya tunaomba mtusaidie katika kuhamasisha waamini mbalimbali ili waweze kujiunga na kwaya yetu na pia kutusaidia mawazo mbalimbali ya kujikwamua kiuchumi.


  1. MWISHO

Tunatoa shukrani zetu nyingi za dhati Kwako Mgeni Rasmi, Baba Paroko, Mapadre, Walezi na Marafiki wote kwa moyo wenu wa kujitoa na kushiriki nasi katika Tafrija hii fupi. Tunasema Asante na tunawatakia Matashi Mema na Mungu awabariki Sana.

WENU KATIKA UTUME WA KRISTO.


  Imeandaliwa na                                                                                                          Imeidhinishwa na
…………………………..                                                                                       ……………………………
SIBILINA KIMARO                                                                                              LUAMBANO PATRICK
  Katibu wa kwaya                                                                                                   Mwenyekiti  wa Kwaya






No comments:

Post a Comment

Aleluya Kuu

Jesus Christ Your My Life