|
PAROKIA YA BIKIRA MARIA WA MLIMA
KARMEL - BUNJU
KWAYA YA BIKIRA MARIA WA MLIMA KARMEL
JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM
P. O. Box 167, Dar
es Salaam
MOBILE: +255784
799 455
KATIBA YA KWAYA YA BIKIRA
MARIA WA MLIMA KARMELI.
|
|
UTANGULIZI:
IMANI
Kwaya inaamini kwamba
kwa kuimba vizuri wanakwaya husali na kutangaza neno la Mungu. Pamoja na
kumtukuza Mungu. Pia Mwanakwaya anayeimba vizuri, anasali mara mbili zaidi ya
kawaida.
Katiba hii imueundwa
mwaka 2006. Katiba hii imerekebishwa mwaka 2009 na 2010 kwa mara ya pili.
SEHEMU
YA KWANZA:
1.1 JINA LA KWAYA
(a)
Kwaya hii itaitwa Bikira Maria wa Mlima
Karmeli
(b)
Somo kwa Kwaya Bikira Maria wa Mlima
Karmeli
(c)
Makao makuu ya Kwaya ni kanisa Katoliki
Kigango cha Mt. Joseph Bunju.
1.2 MADHUMUNI YA KWAYA
(a)
Kuwaongoza na kuwashirikisha wakristo
katika ibada ya Misa Takatifu kulingana na taratibu za kiluturujia.
(b)
Kumtukuza na kumsifu Mungu kwa nyimbo
(c)
Kulinda na kudumisha Imani ya Kanisa
Katoliki na moyo wa upendo moyoni mwetu.
(d)
Kueneza na kuhubiri neno la Mungu kwa
nyia ya nyimbo.
(e)
Kujenga na kuimarisha moyo wa upendo
miongozi mwa wanakwaya wakristo wa Parokia yetu na Parokia nyingine.
(f)
Kujenga na kuimarisha uhusiano mwema na
Kwaya nyingine Jimboni, Tnzania nzima na Duniani kote.
1.3 SIFA ZA MWANAKWAYA.
(a)
Mtu yeyote ambaye ni Mkatoliki mwenye
umri usiopungua miaka kumi na tano (15) na kuendelea na mwenye akili timamu
anaweza kujiunga na Kwaya.
(b)
Awe na uwezo wa kuimba na kupenda kuimba.
(c)
Awe mwenye kujiheshimu, asiyefanya
matendo kinyume na maadili ya kikatoliki.
(d)
Awaheshimu viongozi wa kanisa, Viongozi
wa Kwaya na wanakwaya wenzake
(e)
Awe asiyetengwa na kanisa Katoliki au
kuwa na kizuizi chochote cha Sakramenti au iwapo anacho basi awe katika
jitihada za kuondokana nacho.
1.4 MASHARTI YA KWAYA
(a)
Usajili – Muda wa usajili ni miezi
mitatu(3) baada ya hapo atasajiliwa au kutosajiliwa kutokana na mwenendo wake,
anaweza kuongezewa muda wa usajili kwa maandishi.
(b)
Siku za mazoezi zifuatwe ipasavyo yaani
Jumanne, Ijumaa na Jumamosi kuanzia saa 11:00 jioni hadi saa 12:30 jioni,
pamoja na misa za jumapili na siku nyingine za dharula.
(c)
Asiyehudhuria mazoezi kwa wiki nzima
akae nyuma ya benchi la Kwaya.
(d)
Hapatakuwa na mchango binafsi-mchango
unaotolewa na mwanakwaya asuichukulie kwamba anajiwekea akiba
(e)
Mwanakwaya akishindwa kuhudhuria kwenye
Kwaya atapewa onyo la mdomo wiki mbili, zaidi ya wiki mbili atapewa barua,
ikiwa unashindwa kwa zaidi ya mwezi andika barua.
1.5 MASHARTI YA MWANAKWAYA
(a)
Mwanakwaya atakaye shindwa kuhudhuria au
kuwa karibu na kikundi bila taarifa maalumu ndani ya mwezi mmoja(1) ataandikiwa
barua ya kumtaka ajieleze au ya kumpa onyo au atasimsmishwa.
(b)
Mwanakwaya akiwa na nidhamu mbaya ndani
na nje ya kikundi(atasimamishwa au kufukuzwa)
(c)
Mwankwaya akiwa ni chanzo cha vikwazo
vingi ndani ya kikundi mf. Lugha chafu zinazoleta mvurugano katika kikundi,
ataadhibiwa kikatiba.
(d)
Mwanakwaya atasimamishwa kujihusisha na
uimbaji anapopatikana na tuhuma ndani na nje ya Kwaya, uchunguzi ukikamilika
ataarifiwa kuendelea au kutoendelea na Kwaya.
(e)
Mwanakwaya analazimika kutoa michango
yote husika katika Kwaya.
1.6 WAJIBU WA MWANAKWAYA
(a)
Mwanakwaya anawajibika kushiriki
kikamilifu katika shughuli zote za Kwaya kufuatana na utaratibu uliowekwa kwa
mujibu wa katiba hii.
(b)
Kuhudhuria ibada na hafla zote
zitakazoihusisha Kwaya hii.
(c)
Kuwa tayari kujikosoa, kukosoa na
kukosolewa.
(d)
Kuwa
mfano wa tabia njema na upendo kwa wote.
(e)
Kuhudhuria mazoezi bila kukosa.
(f)
Kila mwanakwaya anawajibika kwa kutunza
mali za Kwaya mf. Sare
(g)
Kurudisha mali za Kwaya pale anapoacha
au kuhama.
(h)
Kuwa na sare(kujinunulia sare)
zilizonunuliwa kwa ubinafsi, sare zilizonunuliwa na Kwaya atagawiwa.
(i)
Kuheshimu sare za Kwaya na siyo kuvaa
hovyo hovyo.
(j)
Kulipa ada na michango husika.
1.7 HAKI ZA MWANAKWAYA
Mwanakwaya ana haki ya:-
(a)
Kuwa huru kutoa malalamiko, shida au
kujitetea iwapo ametuhumiwa, atafanya hivyo katika kikao kinachohusika pindi atakaporuhusiwa
kufanya hivyo.
(b)
Kuongea na Kiongozi yeyote juu ya
malalamiko kwa kufuata taratibu zilizopangwa.
(c)
Kufahamu mapato na matumizi ya Kwaya
(d)
Kuchagua au Kuchaguliwa kuwa kiongozi wa
Kwaya.
(e)
Kutoa maoni yake pale anapohusika.
1.8 KUSIMAMISHWA KWAYA
Mwanakwaya atasimamishwa kuendelea na
Kwaya:-
(a)
Endapo ameonekana kuwa na kizuizi cha
muda mrefu ambacho hayuko katika hatua za kuondokana nacho.
(b)
Endapo kiongozi au mwanakwaya yeyote
atatumia vibaya fedha za Kwaya bila idhini ya Kwaya, pia atatakiwa kulipa fidia
ya fedha atakazokuwa anadaiwa kulingana na maamuzi ya kikao cha Kwaya.
NB
·
Kabla ya kusimamishwa apewe onyo mara
tatu, onyo la kwanza kwa mdomo la pili kwa barua na baadaye atasimamishwa rasmi
kwa barua.
·
Kmati tendaji iwashauri wale wenye
vizuzi kisakramenti ili waondokane navyo.
1.9 KUACHA KWAYA
Mwanakwaya anaweza kuacha Kwaya iwapo:-
(a)
Atatoa taarifa ya kimaandishi kwenye
Kwaya kwa sababu zake zilizo na msingi, taarifa atoe mwezi mmoja kabla.
(b)
Mwanakwaya anaumwa au kufariki
2.0
KUACHISHWA KWAYA
Mwanakwaya ataachishwa
Kwaya :-
(a)
Ikiwa hatatimiza wajibu wake kama
mwanakwaya na masharti ya Kwaya ipasavyo
(b)
Ikiwa atapatikana na makosa makubwa ya
kinidhamu ndani na nje ya Kwaya
(c)
Kwa makosa yenye uzito wa kawaida,
mwanakwaya aliyefanya kosa mara tatu(3) kabla ya kuachishwa , makosa na maonyo
yatatumwa katika kipindi cha miezi sita(6)
(d)
Mwanakwaya atakayepatikana na makosa
madogomadogo atachukuliwa hatua na kamati ya nidhamu kwa kuonywa kwa mdodmo, na
mara ya pili ataandikiwa barua na nafasi ya kujieleza na ya tatu kamati tendaji
itatoa maamuzi ya mwisho.
(e)
Kwa makosa ya hali ya juu yenye kuleta
fedheha kwa Kwaya, mwanakwaya aliyefanya kosa atafukuzwa mara moja.
2.1 SEHEMU YA PILI: MUUNDO WA
UONGOZI
2.1. KIONGOZI
Kiongozi
wa Kwaya ni mwanakwaya yeyote mwenye dhamana yoyote aliyechaguliwa au kuteuliwa
kikatiba.
Imekaa vizur nilitaka kujua majukumu ya mwalim wa kwaya
ReplyDeleteNzuri
ReplyDelete